1. Inhalt
  2. Navigation
  3. Weitere Inhalte
  4. Metanavigation
  5. Suche
  6. Choose from 30 Languages
Wrong language? Change it here. DW.DE has chosen Kiswahili as your language setting.
  • Karikatur von den südafrikanischen Künstlern John Swanepoel und John Curtis (Foto: DWJN)

    Katuni za Umoja wa Afrika

    Tuzo ya kwanza ya AU bila ya magurudumu

    Katuni iliyopewa jina " Je tumeshafika?" imechorwa na mchoraji wa Afrika Kusini John Swanepoel na Jonh Curtis. Katika nchi yao wanajulikana kama "Dr. Jack & Curtis." Wachoraji hao wameshika nafasi ya kwanza katika shindano la tatu kwa mwaka huu la uchoraji katuni la Ujerumani " Third World Journalist Net" Kwa mwaka huu, mada kuu ya shindano hilo la kimataifa ilikuwa "Miaka 50 ya umoja wa Afrika"

  • Karikatur von Victor Ndula aus Kenia (Foto: DWJN)

    Katuni za Umoja wa Afrika

    Tundu katika sehemu ya pili

    "Umoja ni muhimu kwa kudumisha Afrika." Hivyo ndivyo ambavyo Victor Ndula kutoka Kenya alivyoupa mchoro wake jina. Alipata nafasi ya katika shindano la kuchora katuni.

  • Karikatur von Samuel Mwamkinga aus Tansania (Foto: DWJN)

    Katuni za Umoja wa Afrika

    Namba tatu: Mvutano

    Samuel Mwamkinga kutoka Tanzania amekuwa mshindi wa tatu. Mchoro wake umeweka wazi changamoto za Umoja wa Afrika.

  • Karikatur von Ssentongo Jimmy Spire aus Uganda (Foto: DWJN)

    Katuni za Umoja wa Afrika

    Mbwa anaebwaka hawezi kuuma

    Baadhi ya washiriki wa mashindano hayo wanaonesha nafasi ya Afrika katika siasa za kimataifa. Miongoni mwa hao ni Ssentongo Jimmy Spire kutoka Uganda aliechora katuni iliyoitwa "Muungano kwa ajili ya usemi"

  • Karikatur von Junior Heritier Bilaka aus der Demokratischen Republik Kongo (Foto: DWJN)

    Katuni za Umoja wa Afrika

    Mzigo mzito

    Mchoro wa Junior Heritier Bilaka kutoka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo vilevile unaelezea ushawishi mataifa yenye nguvu duniani kwa wanasiasa wa Afrika.

  • Karikatur von Tayo Fatunla aus Nigeria (Foto: DWJN)

    Katuni za Umoja wa Afrika

    Kwa mwendo wa Konokono

    Mtazamo wa Tayo Fatunia kwa maadhimisho ya miaka 50 ya Umoja wa Afrika sio mzuri.

  • Karikatur von Dick Esale, Demokratische Republik Kongo (Foto: DWJN)

    Katuni za Umoja wa Afrika

    Afrika motoni

    Picha hii imechorwa na Dick Esale kutoka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo.

  • Karikatur von Guelajo Silá, Guinéa Bissau (Foto: DWJN)

    Katuni za Umoja wa Afrika

    Hatma ya kupendeza

    Guelajo Sile kutoka Guinea Bissau miongoni mwa washiriki wachache katika shindano hilo ambae ameonesha mtazamo chanya kwa Afrika. Anaamini kwamba mwaka wa 2013 ni "Mwaka wa Afrika" na kauli hiyo ndio imebeba jina la mchoro wake.

  • Karikatur von Haswel Kunyenje, Malawi (Foto: DWJN)

    Katuni za Umoja wa Afrika

    Upya wenye mizizi ya zamani

    Hivi ndivyo ambavyo Haswel Kunyunye kutoka malawi alivyoweza kuuelezea iliyokuwa Umoja wa nchi huru za Afrika (OAU) mpaka sasa Umoja wa Afrika (AU)

  • Karikatur von Michaël Maloji M., Demokratische Repubik Kongo
(Foto: DWJN)

    Katuni za Umoja wa Afrika

    Africa ni kirago chenye viraka

    Mchora katuni kutoka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo Michael Maloji M. Anaonesha mtazamo wake kuhusu Afrika

  • Karikatur von Siphiwo Sobopha S. Sobopha, Südafrika (Foto: DWJN)

    Katuni za Umoja wa Afrika

    Msingi wa Umoja

    "Miguu ya Afrika" ni jina la kielelelezo kilichowasilishwa na Siphiwo Sobopha kutoka Afrika Kusini. Michoro zaidi ya katuni inapatikana katika www.cartoon-competition.org.


    Mwandishi: Maja Braun/es | Mhariri: Susan Houlton

Unaweza kusikiliza matangazo yetu hapa

Kusikiliza matangazo ya Idhaa ya Kiswahili ya DW, tafadhali bonyeza alama ya spika ya masikioni hapo chini, na kuwasiliana nasi, tafadhali tuandikie moja kwa moja kupitia: kiswahili@dw.de.