Katuni iliyopewa jina " Je tumeshafika?" imechorwa na mchoraji wa Afrika Kusini John Swanepoel na Jonh Curtis. Katika nchi yao wanajulikana kama "Dr. Jack & Curtis." Wachoraji hao wameshika nafasi ya kwanza katika shindano la tatu kwa mwaka huu la uchoraji katuni la Ujerumani " Third World Journalist Net" Kwa mwaka huu, mada kuu ya shindano hilo la kimataifa ilikuwa "Miaka 50 ya umoja wa Afrika"
Katuni za Umoja wa Afrika
Tundu katika sehemu ya pili
"Umoja ni muhimu kwa kudumisha Afrika." Hivyo ndivyo ambavyo Victor Ndula kutoka Kenya alivyoupa mchoro wake jina. Alipata nafasi ya katika shindano la kuchora katuni.
Katuni za Umoja wa Afrika
Namba tatu: Mvutano
Samuel Mwamkinga kutoka Tanzania amekuwa mshindi wa tatu. Mchoro wake umeweka wazi changamoto za Umoja wa Afrika.
Katuni za Umoja wa Afrika
Mbwa anaebwaka hawezi kuuma
Baadhi ya washiriki wa mashindano hayo wanaonesha nafasi ya Afrika katika siasa za kimataifa. Miongoni mwa hao ni Ssentongo Jimmy Spire kutoka Uganda aliechora katuni iliyoitwa "Muungano kwa ajili ya usemi"
Katuni za Umoja wa Afrika
Mzigo mzito
Mchoro wa Junior Heritier Bilaka kutoka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo vilevile unaelezea ushawishi mataifa yenye nguvu duniani kwa wanasiasa wa Afrika.
Katuni za Umoja wa Afrika
Kwa mwendo wa Konokono
Mtazamo wa Tayo Fatunia kwa maadhimisho ya miaka 50 ya Umoja wa Afrika sio mzuri.
Katuni za Umoja wa Afrika
Afrika motoni
Picha hii imechorwa na Dick Esale kutoka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo.
Katuni za Umoja wa Afrika
Hatma ya kupendeza
Guelajo Sile kutoka Guinea Bissau miongoni mwa washiriki wachache katika shindano hilo ambae ameonesha mtazamo chanya kwa Afrika. Anaamini kwamba mwaka wa 2013 ni "Mwaka wa Afrika" na kauli hiyo ndio imebeba jina la mchoro wake.
Katuni za Umoja wa Afrika
Upya wenye mizizi ya zamani
Hivi ndivyo ambavyo Haswel Kunyunye kutoka malawi alivyoweza kuuelezea iliyokuwa Umoja wa nchi huru za Afrika (OAU) mpaka sasa Umoja wa Afrika (AU)
Katuni za Umoja wa Afrika
Africa ni kirago chenye viraka
Mchora katuni kutoka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo Michael Maloji M. Anaonesha mtazamo wake kuhusu Afrika
Katuni za Umoja wa Afrika
Msingi wa Umoja
"Miguu ya Afrika" ni jina la kielelelezo kilichowasilishwa na Siphiwo Sobopha kutoka Afrika Kusini. Michoro zaidi ya katuni inapatikana katika www.cartoon-competition.org.
Mwandishi: Maja Braun/es
| Mhariri: Susan Houlton
Unaweza kusikiliza matangazo yetu hapa
Kusikiliza matangazo ya Idhaa ya Kiswahili ya DW, tafadhali bonyeza alama ya spika ya masikioni hapo chini, na kuwasiliana nasi, tafadhali tuandikie moja kwa moja kupitia: kiswahili@dw.de.